Kitu Kipya chini ya Jua

Kutoka Gospel Translations Swahili

Related resources
More By R.C. Sproul Jr.
Author Index
More About Culture
Topic Index
About this resource
English: Something New Under the Sun

© Ligonier Ministries

Share this
Our Mission
This resource is published by Gospel Translations, an online ministry that exists to make gospel-centered books and articles available for free in every nation and language.

Learn more (English).
How You Can Help
If you speak English well, you can volunteer with us as a translator.

Learn more (English).

By R.C. Sproul Jr. About Culture
Part of the series Tabletalk

Translation by Kelvin Odhiambo

Review You can help us improve by reviewing this translation for accuracy. Learn more (English).



Hebu fikiria kama ungalikuwa mwenye nguvu zaidi duniani.Sasa fikiria kama wewe pia ndiye tajiri kuliko watu wote duniani. Je, msingi wa maisha yako ungekuwa tofauti? Je, kila kitu ambacho ni cha kawaida maishani mwako yangeweza kuwa ya kupindukia?Lakini si kuligana na mtu hekima kuliko wote duniani.Mfalme Sulemani alitawala wakati ule Israeli ulikuwa kileleni mamlakani.Israeli wakati huo ulikuwa nguvu ya dunia, mipaka yake pia ilienea. Suleiman vivyo hivyo alifurahia mali ya Croesus ( mfalme tajiri wa Kigiriki ). Hakuna mtu katika dunia alikuwa tajiri kama Sulemani. Bora kuliko yote hii, alikabidhiwa kipawa cha hekima na Mungu wa mbingu na nchi.Kwa hiyo hekima, na kupitia kila aina ya anasa, kila upotovu unaotokona na dunia ,alitamka hivi: "Hakuna kitu kipya chini ya jua" (Mhubiri 1:09).

Ulimwengu mpya ya kishujaa, chini ya mwanga na kengele uvumao, ni ulimwengu huo mmoja tangu kitambo, ni ile ulimwengu moja tangu kitambo. Hii si kumaanisha tusijihadhari na mabadiliko ya kiutamaduni.Baada ya yote haya ni wito wetu kutambua nyakati.Lakini hiyo ni hoja mwafaka.Tunaweza tu kufahamu upepo wa mabadiliko ya wakati tukiwa kwa mlingoti ya mambo ya kudumu. Kutembea imara kati ya mchanga wa kuteleza hatutafuta kuielewa Bali tunatamani miguu yetu kuwa kwenye mwamba.Hapo, na hapo tu basi, tutaimba wimbo mpya.

Kuwa jasiri dunia mpya ni ulimwengu wa kale timid haina maana, kwa hiyo, tuweze kushikilia ukweli wa zamani.Haijalisi vile teknolojia ina badilika, haitaweza kubadilisha kweli hizi halisi - kwamba sisi, ndani yetu, ni wenye dhambi wenye vita na Mungu mwenyewe. Haijalishi vile ukweli unapokelewa na tamaduni, ukweli ni kwamba Yeye alimtuma Mwana wake wa pekee ili kila mtu amwaminiye asipotee bali awe na uzima wa milele.Haijalishi vile ulimwengu utakuwa imechanyikiwa ,Yeye bado ana dunia nzima mikononi mwake. Na pia haijalishi vile utamaduni utakuwa umemwasi Mfalme wake wa haki,yatufaa kuwa wenye furaha,tukikumbuka ya kwamba tayari amekabiliana na dunia.

Ushindi wake, hata hivyo, si tu kwa sababu ya furaha yetu ; inaonyesha pia mikakati yetu. Kama magurudumu yangalitoka duniani , kama haya mabadiliko yangekuwa mapya chini ya Jua, basi tunaweza kuelewa majaribu ya kubadilisha mkondo, kukabiliana, kuwa makini na kufuata mkondo.Kama Yesu anatawala sasa, akituma Roho Yake duniani kote, Akiamrisha Neno lake kama upanga wenye makali kuwili, basi tunaweza kukaa na mpango. Tunaweza kuendelea, kwa ajili amekabidhiwa mamlaka yote mbinguni na duniani.Na kwa mamlaka hii ametuamrisha kwenda na kufanya wafuasi kwa mataifa, tukiwabatiza kwa jina la Baba, na la Mwana, na Roho Mtakatifu, na kuwafundisha kuyatii yote alivyotuamuru. Tunaweza kuishi katika imani, tukikumbuka kwamba Yeye yu pamoja nasi hata kama tunakumbwa na shida - hata mwisho wa dunia.

CS Lewis alikuwa si tu mwandishi wa kidini bali msomi wa fasihi ya Kiingereza. Wakati wa kilele cha Vita ya Pili ya Dunia, yeye aliandika insha ambapo aliuliza kwa nini, katikati ya mapambano makubwa kama kati ya wema na uovu , ingekuwa kupoteza wakati kusoma fasihi. Kisha alifafanua kwamba wale waliokataa kufikiri juu ya masuala ya utamaduni hawatakuwa bila utamaduni bali na utamaduni mbaya. Utamaduni hauepukiki, katika vita na kwa amani. Hakuna mtu anaweza kuiweka kando kwa muda kushughulika na mambo muhimu. Hali kadhalika, tukiaamini kwamba utamaduni mpana ni mambo yasiyotuhusu,hatuwezi ipuuza bali kukubaliana nayo. Wale ambao wanapuuza utamaduni watarudia kuiangamiza tena. Kama hatuwezi kurekebisha utamaduni kwa ajili ya injili, kupuuza utamaduni,tunafanya nini?Tunatafuta kwanza ufalme wa Mungu na uadilifu wake. Tunajenga utamaduni kwa mazingira na kwa uongozi wa Kristo kuliko vitu vyote.Tunaishi maisha yetu, kama vile inawezekana, kwa amani na utulivu na watu wote, ambao ni moja na wakati huo huo, Alishambulia kwa nguvu zake milango ya jahannamu.Tunapokataa kufuata mkondo wa utamaduni mpana lakini badala yake kuishi maisha rahisi,maisha ya kiinjili; kama tunavyolea watoto wetu katika nidhamu na mafundisho ya Bwana,tunapohisi njaa na kiu ya haki, tunapotafakari mchana na usiku juu ya amri Yake na kufurahi mchana na usiku juu ya neema Yake, kwa ghafla dunia inapungua mwendo. Mioyo yetu inatulia.Tumetulia tuli, na tunajua kwamba Yeye ni Mungu.

Hakuna kitu chochote mpya chini ya jua. Lakini kila siku, mambo mapya yanaletewa chini ya Mwana. Mbegu ya haradali inaota.Chachu kiasi kigodo kinafanya kazi kwa donge kubwa la ngano. Mwamba, usioguswa kwa mikono ya binadamu, inaenea duniani kote, na Injili ya Bwana Yesu Kristo inajaza dunia kama maji inavyojaza bahari.