Je, Kwa Nini Kristo Alikufa Msalabani?/Kristo alikufa kuharibu uadui kati ya makabila za ulimwengu

Kutoka Gospel Translations Swahili

(Tofauti baina ya masahihisho)
 
Mstari 1: Mstari 1:
{{info|Fifty Reasons Why Jesus Came to Die/To Destroy the Hostility Between Races}}<br>  
{{info|Fifty Reasons Why Jesus Came to Die/To Destroy the Hostility Between Races}}<br>  
<blockquote>
<blockquote>
-
''“Wewe unastahili kukitwaa kitabu na kuzivunja lakiri zake, kwa<br> sababu ulichinjwa na kwa damu Yako ukamnunulia Mungu watu<br> kutoka katika kila kabila, kila lugha, kila jamaa na taifa “<br> (Ufunuo 5:9)''
+
''“Kwa maana Yeye mwenyewe ndiye amani yetu, aliyetufanya sisi<br> tuliokuwa wawili, yaani, Wayahudi na watu wa Mataifa tuwe<br> wamoja kwa kuvunja kizuizi na kubomoa ule ukuta wa uadui<br> uliokuwa kati yetu. Kwa kuibatilisha ile sheria pamoja na amri<br> zake na maagizo yake alipoutoa mwili wake, ili apate kufanya<br> ndani yake mtu mmoja mpya badala ya hao wawili, hivyo,<br> akifanya amani” (Waefeso 2:14-16).''
</blockquote>
</blockquote>
-
Katika mstari huu tunatazama kile ambacho kinatendeka mbinguni. Mtume Yohana alikubaliwa kuona kile ambacho kitakuwa kikitendeka huku mbinguni milele. “Kisha nikaona katika mkono Wake wa kuume yule aliyeketi kwenye kiti cha enzi, kitabu kilichoandikwa ndani na upande wa nyuma kikiwa kimefungwa kwa lakiri saba.” (Ufunuo 5:1). Muhuri ni hesabu ya kila kitu ambacho kitatendeka hapa ulimwenguni. Moja wa malaika alimwambia Yohana, “Simba wa kabila la Yuda, wa uzao wa Daudi, ameshinda, ili kwamba aweze kukifungua hicho kitabu na kuvunja hizo lakiri zake saba” (Ufunuo 5:5). Simba wa kabila la Yuda ni Kristo Yesu. Ameshinda kifo, kwa kifo chake na kufufuka kwake. Yohana alimwona, “Mwana-Kondoo amesimama, akiwa kama amechinjwa” (Ufunuo 5:6).  
+
Katika Agano Jipya tunasoma kuwahusu Wayahudi na watu wa Mataifa. Ni wazi kwamba kulikuwepo uadui kati ya watu hawa. Mfano wa haya ni katika kitabu cha Wagalatia 2:11-12, “Lakini Petro alipofika Antiokia, mimi nilimpiga ana kwa ana kwa sababu alikuwa amekosa kwa wazi. Kabla baadhi ya watu waliotoka kwa Yakobo hawajafika, alikuwa akila pamoja na watu wa Mataifa. Lakini hao watu walipofika alianza kujiondoa na kujitenga na watu Mataifa kwa sababu aliwaogopa wale wa kundi la tohara.
-
Malaika wote waliaanguka chini na kuanza kumwabudu. Waliimba wimbo mpya wakisema kwamba kwa sababu Kristo Yesu alikufa, ako na uwezo wa kufungua muhuri wa kihistoria. Kile malaika hawa wanamaanisha ni kwamba, kwa sababu ya kifo cha Bwana Yesu Kristo, sasa Yeye ndiye Bwana wa kihistoria: Yeye anadhibiti kila kitu ambacho kinatendeka hapa ulimwenguni. Nao waimba wimbo mpya wakisema, “Wewe unastahili kukitwaa kitabu na kuzivunja lakiri zake, kwa sababu ulichinjwa na kwa damu Yako ukamnunulia Mungu watu kutoka katika kila kabila, kila lugha, kila jamaa na taifa” (Ufunuo 5:9).  
+
Kefa (yaani Petro) alikuwa akiishi katika uhuru wa Kristo hata kama alikuwa Myahudi. Alikuwa akila na watu wa mataifa kwa sababu kwake hakukuwa na uadui kati yake na watu wa mataifa ambao walikuwa wameokoka. Lakini wakati Wayahudi ambao walishikilia desturi sana walikuja Antiokia, Kefa aliwaogopa sana. Kwa hivyo aliacha kula na watu wa mataifa na akawa sasa anakula tu na Wayahudi pekee. Aliogopa kwamba wale Wayahudi ambao walikuwa wamekuja Antiokia wangemkemea sana.  
-
Kristo alikufa kuwaokoa watu wa aina tofauti kutoka kila taifa la ulimwenguni. Watu wa ulimwengu wametenda dhambi. Kila taifa ulimwenguni linahitaji wokovu. Hii ndiyo sababu Yesu Kristo alikuja ulimwenguni: alikuja kuwaokoa watu kutoka kila taifa la ulimwengu. Ugonjwa wa dhambi uko kila mahali na tabibu pia wa ugonjwa huu ako kila mahali. Kristo Yesu alisema, “Lakini Mimi, nikiinuliwa kutoka katika nchi, nitawavuta watu wote waje Kwangu.” (Yohana 12:32). Msalabani Yesu Kristo alikufa kwa ajili ya watu kutoka kila taifa la ulimwengu.  
+
Wakati Paulo aliona yale ambayo yalikuwa yametendeka, alikasirika kwa sababu ya tabia ya Kefa. Siyo jambo jema machoni pa Mungu mkristo kukataa kushiriki na mkristo mwingine kwa sababu ya kabila. Wakati Paulo aliona ni nini inatendeka, aliongea na Kefa uso kwa uso kumrekebisha kuhusu mambo haya (Wagalatia 2:14). Wale wote ambao wako na ukabila wanakataa ujumbe wa injili. Wakati Kefa alikataa kushiriki na wakristo wa mataifa alikuwa anakataa ujumbe wa injili. Kristo alikufa kwa ajili ya watu wake wote na kwa hivyo hatufai kuwa na ukabila miongoni mwetu.  
-
Ukristo ulianza katika nchi ya Uisraeli na baadaye ukaenea bara Uropa. Sasa imeenea katika kila pembe la ulimwengu. Katika Agano la kale tunaambiwa kwamba hili jambo lilikuwa litendeke: “Miisho yote ya dunia watasherehekea na kuabudu, wote waendao mavumbini watapiga magoti mbele yake, wote ambao hawawezi kudumisha uhai wao.” (Zaburi 22:27). “Mataifa yote wafurahi na kuimba kwa shangwe, kwa kuwa unatawala watu kwa haki na kuongoza mataifa ya dunia” (Zaburi 67:4). Kwa hivyo wakati huduma wa Kristo Yesu ulifika kilele hapa ulimwenguni, alitangaza mpango wake wazi wazi: “Haya ndiyo yaliyoandikwa: Kristo atateswa na siku ya tatu atafufuka kutoka kwa wafu. Toba na msamaha wa dhambi utatangazwa kupitia Jina Lake, kuanzia Yerusalemu” (Luka 24:46-47). “Kwa sababu hii, enedeni ulimwengu mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi” (Mathayo 28:19).  
+
Kwa hivyo wakati Paulo aliona kile ambacho kilikuwa kikifanywa na Kefa, alizungumza mbele ya watu kwamba, “Wewe ni Myahudi, nawe unaishi kama mtu wa Mataifa na wala si kama Myahudi. Imekuwaje basi, mnawalazimisha watu Mataifa kufuata desturi za Kiyahudi?” (Wagalatia 2:14). Wakati Kefa alikataa ushirika na watu wa mataifa alikuwa akisema, lazima muwe Wayahudi ndipo niweze kushiriki nanyi. Ni kama mtu leo aseme, lazima uwe mtu wa kabila yangu ndipo uwe mshirika wa kanisa langu. Lakini Bwana Yesu Kristo aliondoa mambo haya yote wakati alipokufa msalabani.  
-
Bwana Yesu Kristo siyo mwokozi tu wa mataifa fulani au makabila fulani. Yeye si wa taifa moja pekee. “Tazama, Mwana Kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu!” (Yohana 1:29). “Kwa maana hakuna tofauti kati ya tofauti kati ya Myahudi na Myunani, Yeye ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao. Kwa maana, ‘Kila mtu atakayeliita Jina la Bwana, ataokoka’ ” (Warumi 10:12-13). Mwite sasa na ungane na watu wake ambao wako katika kila pembe la ulimwengu.
+
Kristo alikufa ili makabila ya ulimwengu yapatanishwa kwake. Anawaleta pamoja watu wake wote, haijalishi wanatoka katika kabila gani au rangi gani au nchi gani, wote ni wake.  
 +
 
 +
Utenganisho ambao uko katika ulimwengu kote ni kati ya wale ambao wameokoka na wale ambao hawajaokoka. Wale wote ambao wameokoka ni wa Mungu na ni watoto wake wapendwa. Wale wote ambao hawajaokoka ni wa shetani. Watu hawa hawako katika ufalme wa Mungu na hawataingia mbinguni wakati watakapokufa. Kristo Yesu ndiye njia ya pekee mtu yeyote anaweza kuingia ufalme wa Mungu.

Toleo lililopo 17:58, 11 Agosti 2011

Related resources
More By John Piper
Author Index
More About The Death of Christ
Topic Index
About this resource
English: Fifty Reasons Why Jesus Came to Die/To Destroy the Hostility Between Races

© Desiring God

Share this
Our Mission
This resource is published by Gospel Translations, an online ministry that exists to make gospel-centered books and articles available for free in every nation and language.

Learn more (English).
How You Can Help
If you speak English well, you can volunteer with us as a translator.

Learn more (English).

By John Piper About The Death of Christ
Chapter 44 of the book Je, Kwa Nini Kristo Alikufa Msalabani?

Translation by Desiring God


“Kwa maana Yeye mwenyewe ndiye amani yetu, aliyetufanya sisi
tuliokuwa wawili, yaani, Wayahudi na watu wa Mataifa tuwe
wamoja kwa kuvunja kizuizi na kubomoa ule ukuta wa uadui
uliokuwa kati yetu. Kwa kuibatilisha ile sheria pamoja na amri
zake na maagizo yake alipoutoa mwili wake, ili apate kufanya
ndani yake mtu mmoja mpya badala ya hao wawili, hivyo,
akifanya amani” (Waefeso 2:14-16).

Katika Agano Jipya tunasoma kuwahusu Wayahudi na watu wa Mataifa. Ni wazi kwamba kulikuwepo uadui kati ya watu hawa. Mfano wa haya ni katika kitabu cha Wagalatia 2:11-12, “Lakini Petro alipofika Antiokia, mimi nilimpiga ana kwa ana kwa sababu alikuwa amekosa kwa wazi. Kabla baadhi ya watu waliotoka kwa Yakobo hawajafika, alikuwa akila pamoja na watu wa Mataifa. Lakini hao watu walipofika alianza kujiondoa na kujitenga na watu Mataifa kwa sababu aliwaogopa wale wa kundi la tohara.”

Kefa (yaani Petro) alikuwa akiishi katika uhuru wa Kristo hata kama alikuwa Myahudi. Alikuwa akila na watu wa mataifa kwa sababu kwake hakukuwa na uadui kati yake na watu wa mataifa ambao walikuwa wameokoka. Lakini wakati Wayahudi ambao walishikilia desturi sana walikuja Antiokia, Kefa aliwaogopa sana. Kwa hivyo aliacha kula na watu wa mataifa na akawa sasa anakula tu na Wayahudi pekee. Aliogopa kwamba wale Wayahudi ambao walikuwa wamekuja Antiokia wangemkemea sana.

Wakati Paulo aliona yale ambayo yalikuwa yametendeka, alikasirika kwa sababu ya tabia ya Kefa. Siyo jambo jema machoni pa Mungu mkristo kukataa kushiriki na mkristo mwingine kwa sababu ya kabila. Wakati Paulo aliona ni nini inatendeka, aliongea na Kefa uso kwa uso kumrekebisha kuhusu mambo haya (Wagalatia 2:14). Wale wote ambao wako na ukabila wanakataa ujumbe wa injili. Wakati Kefa alikataa kushiriki na wakristo wa mataifa alikuwa anakataa ujumbe wa injili. Kristo alikufa kwa ajili ya watu wake wote na kwa hivyo hatufai kuwa na ukabila miongoni mwetu.

Kwa hivyo wakati Paulo aliona kile ambacho kilikuwa kikifanywa na Kefa, alizungumza mbele ya watu kwamba, “Wewe ni Myahudi, nawe unaishi kama mtu wa Mataifa na wala si kama Myahudi. Imekuwaje basi, mnawalazimisha watu Mataifa kufuata desturi za Kiyahudi?” (Wagalatia 2:14). Wakati Kefa alikataa ushirika na watu wa mataifa alikuwa akisema, lazima muwe Wayahudi ndipo niweze kushiriki nanyi. Ni kama mtu leo aseme, lazima uwe mtu wa kabila yangu ndipo uwe mshirika wa kanisa langu. Lakini Bwana Yesu Kristo aliondoa mambo haya yote wakati alipokufa msalabani.

Kristo alikufa ili makabila ya ulimwengu yapatanishwa kwake. Anawaleta pamoja watu wake wote, haijalishi wanatoka katika kabila gani au rangi gani au nchi gani, wote ni wake.

Utenganisho ambao uko katika ulimwengu kote ni kati ya wale ambao wameokoka na wale ambao hawajaokoka. Wale wote ambao wameokoka ni wa Mungu na ni watoto wake wapendwa. Wale wote ambao hawajaokoka ni wa shetani. Watu hawa hawako katika ufalme wa Mungu na hawataingia mbinguni wakati watakapokufa. Kristo Yesu ndiye njia ya pekee mtu yeyote anaweza kuingia ufalme wa Mungu.