Je, Kwa Nini Kristo Alikufa Msalabani?/Kristo alikufa kujifunza kutii na kukamilishwa

Kutoka Gospel Translations Swahili

Related resources
More By John Piper
Author Index
More About The Death of Christ
Topic Index
About this resource
English: Fifty Reasons Why Jesus Came to Die/To Learn Obedience and Be Perfected

© Desiring God

Share this
Our Mission
This resource is published by Gospel Translations, an online ministry that exists to make gospel-centered books and articles available for free in every nation and language.

Learn more (English).
How You Can Help
If you speak English well, you can volunteer with us as a translator.

Learn more (English).

By John Piper About The Death of Christ
Chapter 3 of the book Je, Kwa Nini Kristo Alikufa Msalabani?

Translation by Desiring God


“Ingawa alikuwa Mwana, alijifunza utii kutokana na mateso
aliyoyapata” (Waebrania 5:8).

“Ili kuwaleta wana wengi katikautukufu, ilimpendeza Mungu,
kwa ajili Yake na kwa kupitia Yeye kila kitu kilichopo,
kumkamilisha mwanzilishi wa wokovu wao kwa njia ya mateso”
(Waebrania 2:10).

Katika kitabu cha Waebrania tunaambiwa kwamba Kristo alijifunza kutii kupitia kwa mateso na pia “alifanywa mkamilifu” kupitia kwa mateso. Pia katika kitabu hicho hicho tunaambiwa kwamba Kristo alikuwa bila dhambi: “Yeye mwenyewe alijaribiwa kwa kila namna, kama sisi tujaribiwavyo, lakini Yeye hakutenda dhambi” (Waebrania 4:15).

Hivi ndivyo tunafunzwa katika Biblia kwamba Kristo hakuwa na dhambi kamwe. Tunaambiwa kwamba alikuwa Mwana Mtakatifu wa Mungu. Pia tunaambiwa alikuwa mwanadamu kamili na alipata majaribu na mateso mengi na kupitia mambo mengi magumu kama yale kila mwanadamu anapata katika maisha. Kuna wakati Yesu Kristo alikuwa na njaa (Mathayo 21:18), kuna wakati mwingine Yesu Kristo alikasirika na kuhuzunika (Marko 3:5), na pia kuna wakati mwingine Yesu Kristo alihisi uchungu (Mathayo 17:12). Yesu Kristo alikuwa mwanadamu kamili kama wanadamu wa kawaida, lakini Mungu alimpenda sana kwa upendo mkamilifu: “Yeye hakutenda dhambi, wala udanganyifu haukuonekana kinywani mwake” (1 Petro 2:22).

Kwa hivyo, wakati Biblia inasema kwamba, “alijifunza kutii kupitia mateso,” haimaanishi kwamba wakati mwingine Yesu hakuwa akitii na alijifunza kutii baada ya kupitia mateso. Bali inamaanisha kwamba wakati alikuwa akikumbwa na matatizo alifahamu inamaanisha nini kwa watu wa kawaida kutii neno la Mungu. Wakati tunaambiwa Yesu, “alifanywa mkamilifu kupitia mateso “ haimaanishi kwamba hakuwa mkamilifu hadi alipopitia mateso ndiyo akawa mkamilifu. Tunajua kwamba Yesu alikuwa mkamilifu kila wakati. Kile Biblia inasema hapa ni kwamba Yesu Kristo alikuwa anatengeneza hesabu kamilifu ili atuokoe.

Hivi ndivyo ilifanyika wakati Yesu alibatizwa. Hakuhitaji ubatizo kwa sababu alikuwa Mwana wa Mungu. Kwa hivyo alimwambia Yohana, “Kubali hivi sasa; kwa maana ndivyo itupasavyo kwa njia hii kuitimiza haki yote” (Mathayo 3:15).

Hivi ndivyo Biblia inafundisha: Yesu Kristo hangepata majaribu na mateso hapa duniani, hangekuwa mwokozi anayestahili kuwaokoa watu wake. Wakati aliteseka na wakati alipata majaribu alijifunza maana ya kuwa mwanadamu. Ni kama mwanasiasa ambaye amezaliwa katika jamii tajiri na amesomea katika shule mzuri na kuenda katika chuo kikuu ng’ambo. Mtu huyu anaweza kumwambia mtu maskini, “Mimi ni mwanadamu kama wewe,” lakini yule maskini anajua kwamba mwanasiasa huyu hawezi kuelewa umaskini ni nini kwa sababu hajawahi kuwa katika hali ya umaskini. Lakini ikiwa ataelewa vyema hali ya kuwa maskini, basi ataweza kumsaidia yule maskini. Jinsi hiyohiyo Yesu alipata mateso na shida mingi ili ajifunze maana ya kuwa mwanadamu anayeishi hapa ulimwenguni. Hivi ndivyo anaweza kuwa mwokozi wetu na anaweza kutuita mandugu na madada (Waebrania 2:17).